Tuesday, October 22, 2019

JINSI YA KUTENGENEZA AJIRA SEHEMU YA KWANZA

Salamu!

Yesu Mwana wa Daudi, Hallelujah x3

JE! UNASHAUKU NA NIA YA KUFANYAKAZI? JE! UNAMAONO YA AJIRA?
“Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri ili kwamba: ‘‘Mtu ye yote asiyetaka kufanya kazi, wala asile.’’ Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine. Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwaonya katika Jina la Bwana Yesu Kristo wafanye kazi kwa utulivu na kujipatia mahitaji ya maisha yao wao wenyewe.” 2 WATHESALONIKE 3:10-12
 “Kwa maana viumbe vyote vinangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa watoto wa Mungu.” WARUMI 8:19

TAFUTA MAKAMPUNI BINAFSI MATATU, MASHIRIKA YA KIMATAIFA, NGO’S, TAASISI ZA UMA, AU SEREKALINI.
“Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. Kwa maana kila aombaye hupewa, naye atafutaye huona, naye abishaye hufunguliwa mlango.” MATHAYO 7:7-8

 ‘ANDIKA BARUA ZA MAOMBI YA KAZI SEHEMU TATU TOFAUTI, AMBATANISHA NA WASIFU WAKO “CV’S”.
“Nitasimama katika zamu yangu na kujiweka mwenyewe juu ya maboma, Nitatazama nione atakaloniambia na    ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili. Jibu La BWANA Kisha BWANA akajibu: Andika ufunuo huu na ukaufanye wazi juu ya vibao ili mpiga mbiu akimbie nao. Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika, unazungumzia mambo ya mwisho na kamwe hautakosea. Iwapo utakawia, wewe usubiri, kwa hakika utakuja na hautachelewa.”HABAKUKI 2:1-3.

CHUKUA HATI YA TABIA NJEMA KUTOKA POLISI.
Msidanganyike, “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.” 1 WAKORINTHO 15:33

PELEKA MAOMBI YAKO YA AJIRA KWA MCHUNGAJI WAKO AU KIONGOZI WAKO WA IMANI AYABARIKI..  
“Mungu akawabariki na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.’’ MWANZO 1:28
“Mungu akaibariki siku ya saba akaifanya takatifu, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kazi zote za kuumba alizokuwa amefanya.” MWANZO 2:3
NENDA UKAFANYE KAZI KIMVULI KATIKA VITUO VYA WATOTO YATIMA ,WAJANE, WAZEE, WATOTO WA MITAANI, KUTEMBELEA WAFUNGWA KUWATIA MOYO, KWANDA HOSPITALINI KUOMBEA WAGONJWA, KUTUNZA MAZINGIRA, NA KUHUBIRI INJILI, CHAGUA KAZI MOJA TU KATIKA HIZO HAPO JUU.
“Dini iliyo safi, isiyo na uchafu, inayokubalika mbele za Mungu Baba yetu, ndiyo hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao na kujilinda usitiwe madoa na dunia.” YAKOBO 1:27

“BWANA Mungu akamchukua huyo mtu akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza” .MWANZO 2:15

“Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea” MATHAYO 25:35-36
“Basi wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda hadi Galilaya kwenye ule mlima ambao Yesu alikuwa amewaagiza. Walipomwona, wakamwabudu, lakini baadhi yao wakaona shaka. Yesu akawajia na kusema, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Kwa sababu hii, enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika Mimi niko pamoja nanyi sikuzote, hadi mwisho wa nyakati.’’ Amen.  MATHAYO 28:16-20


ANZA MAOMBI YA KUOMBEA WATU AMBAO HAWANA KAZI WAPATE KAZI KWA KUSIMAMIA ANDIKO HILI
“Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, BWANA akamfanikisha tena naye akampa mara mbili kama yale aliyokuwa nayo hapo kabla.” AYUBU 42:10


INGIA KWENYE MAOMBI YA TOBA NA REHEMA MARA SABA KWA SIKU 
“Baba Jehovah akusamehe dhambi zako zote  na kuponya magonjwa yako yote, kwa Damu ya Yesu kristo, Kwa maana fadhili zake niza milele katika   jina la Yesu kristo wa Nazareth”  ZABURI 103:3
 “Ee Mungu, unihurumie, kwa kadri ya upendo wako usiokoma  kwa kadri ya huruma  wako usiokoma,yako kuu uyafute makossa yangu yote kwa Damu ya Yesu kristo, Kwa maana fadhili   zake niza milele katika   jina la Yesu kristo wa Nazareth,” ZABURI 51:1

UTAKAPOKUWA UNAJIANDAA KWENDA KATIKA USAILI SIMAMIA MAANDIKO HAYA
‘‘Watakapowapeleka katika masinagogi mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema: Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati uo huo mnachopaswa kusema.” LUKA 12:11-12

ANZA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUPATA AJIRA KILA BAADA YA DAKIKA SITINI LISAA LIMOJA. MUNGU NI ALPHA NA OMEGA 59MINS-60MINS
“Shukuruni kwa kila jambo, kwa  maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.” 1 WATHESALONIKE 5:18

MASOMO HAYA YANATOLEWA BURE KATIKA OFISI ZETU ZA ARUSHA WASILIANA NASI +255 788 71 56 56

SHARE, “WATUMIE NA WENGINE UJUMBE HUU WAPATE KUJIFUNZE NA WAO”.



No comments:

Post a Comment

              2021-MWAKA WA AKILI INAYOPITA MIPAKA Kingdom Business Clubaship  leo Tumeingia Mwaka 2021, Kila Mwaka Tarehe Moja Ya Mwezi Wa ...