Thursday, October 24, 2019

JINSI YA KUTENGENEZA AJIRA SEHEMU YA PILI

Salamu!
Yesu Mwana Wa Daudi, Hallelujah x3

FANYA KAZI KWA MUDA SIYO KWA MIKONO
2 WAKORINTHO 5;7

Tajirika Na Muda - Tumia Muda Kibiashara
Waefeso 5:15-17

Kufanya Kazi Kwa Muda Na Siyo Kwa Mikono Maana Yake Kufanya Kazi Kwa Kutumia  Muda Wako Mwenyewe Wa Masaa 24Hrs Na Kutumia Muda Wa Watu Wengine.  Huwezi Kutajirika Kwa Masaa Yako 24hrs Tu Bali Kwa Kutumia Muda Wa Watu  Wengine.

Ili Uwe Na Muda Zaidi Ya Masaa 24Hrs Chukua Masaa 10Hrs Ya Watu Wengine Kumi(10x10=100) Jumlisha Na Ya Kwako 24Hrs Utakuwa Na Masaa 124Hrs Kwa Siku,  Siyo Masaa 24Hrs Kama Watu Wa Kawaida. UTAJIRI UPO KWENYE MUDA SIYO KWENYE PESA.   
‘’Foolish people use heart to think, But Smart people use brain to think’’.

Tasfiri Ya Kazi Ya Muda Ni Kufikiri, Kutengeneza Ajira, Wazo La Biashara Na Kutafuta Taarifa Kama Vile Unavyosoma Taarifa Hizi.

Wazungu Wanapigana Na Vita Vya Ujinga, Waafrika Wengi Sana Wanapigana Na  Vita Vya Umaskini’. Ukisikia Mtu Ana Kwambia Yule Bwana Ni Mzungu Kwasababu Anatumia Muda Vizuri Anachokisema Ndicho Anachokifanya, Akikuambia Ni Mswahili Basi Kuna Changamoto Hapo. UKISEMA JAPAN UNASEMA MUDA UKISEMA AFRIKA UNASEMA PESA.

Watu Wote Waliofanikiwa Duniani WALIFANYA KAZI ZA MUDA NA SIYO ZA MIKONO! Kuna Aina Mbili Za  Kazi Hapa  Duniani; Kazi Za Muda Zinahitaji Kufikiri Sana.  Kuajiriwa Siyo Kitu Kibaya Bali Ujue Umenyanganywa Uwezo Wa Kufikiri Asilimia 98%.

  •  AKILI KAZI –KUJIAJIRI-  Mungu Anabariki Kazi Ya Akili Yako. 1 KOR 15:34
  •   MKONO KAZI-KUAJIRIWA-Mungu Anabariki Kazi Ya Mkono Wako. KUMB. 28:12

Kazi Zote Zinazofanywa Na Akili Zinafanywa Kwa Muda Na Zile Zinazofanywa Kwa Mikono Zinafanya Kwa Nguvu . Kwa Kuwa Kazi Zote Za Akili Hazi Hitaji Nguvu Wala Vyeti Vya  Chuo Bali Zina Hitaji Muda Tu. Ajira Unayotafuta Leo Ni Ya Aina Gani? Je, Ni Ya Kutumia Muda Au Kutumia Mikono?

Kazi Ya Akili  Unaanzisha Mwenyewe Kwa Kufiri Kwa Kina.Na Hauhitaji Vyeti Ni Ubunifu Tu, Katika Huduma Hii Ya Kingdom Business Clubship Tuna Kufundisha Matumizi Ya Muda Wako Katika Kazi Zote Mbili Kazi Ya Akili Na Kazi Ya Mikono. Kazi Ya Akili Ni Kujiajiri Mwenyewe, Na Kazi Ya Mikono Ni Kuajiriwa. Utakapo Anza Kufikiri Kila Kitu Mwenywe Na Kutumia Akili Yako Asilimia Mia Moja.

Meneja Wa Benki Anatumia Akili Yake Asilimia Mbili Tu  Mama Anayechoma Mahindi Anatumia Akili Yake Asilimia Mia Moja, Kwa Kutafuta Masoko, Kujali Wateja, Matangazo, Nk. Mama Huyu Anafanya Hivi Vyote Mwenyewe. Na Yule Meneja Wa Benki Amerahisishiwa Vitu Kwani Kuna “System” Mfumo Wa Kila Kitu Anakikuta Kazini.

AKILI KAZI NA MKONO KAZI  Ni Kufikiri Kwa Matendo, Yaani Unafikiri Huku Unafanya Hii Ndiyo Njia Peke Yake Inaweza Kumtoa Mtu Katika Umaskini. Muda Unapewa Na Mungu Pesa Unatafuta Mwenyewe, Mungu Anakupa Unachokiitaji, Hakupi Unacho Kitaka. Unahitaji Muda Kutafuta Unacho Kitaka. 1 WAFALME 3:5, MITHALI 30:7-9        

MWISHO WA SEHEMU YA PILI

SEHEMU HII NI YA MAANDIKIKO MATAKATIFU:
“kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.” NEN 2 WAKORINTHO 5:7

“Kwa hiyo iweni waangalifu jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima, 16mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu. Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini yaliyo mapenzi ya Bwana.” NEN  WAEFESO 5:15-17

“Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, msitende dhambi tena, kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.” NEN 1 WAKORINTHO15:34

“BWANA atafungua mbingu, ghala zake za baraka, kukupa mvua kwa majira yake na kubariki kazi zako zote za mkono Wako. Utakopesha mataifa mengi lakini hutakopa kwa ye yote.” NEN KUMBUKUMBU LA TORATI 28:12

 “BWANA akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, ‘‘Omba lo lote utakalo nikupe.’’  NEN 1 WAFALME 3:5

“Ninakuomba vitu viwili, Ee BWANA, usininyime kabla sijafa: Uutenge mbali nami udanganyifu na uongo, usinipe umaskini wala utajiri, bali unipe chakula cha kunitosha kila siku. Nisije nikawa na vingi vya kuzidi nikakukana na kusema, “BWANA ni nani?’’ Au nisije nikawa maskini nikaiba, nami nikaliaibisha jina la Mungu wangu” NEN MITHALI 30:7-9

MASOMO HAYA YANATOLEWA BURE KATIKA OFISI ZETU ZA ARUSHA WASILIANA NASI +255 788 71 56 56

SHARE, “WATUMIE NA WENGINE UJUMBE HUU WAPATE KUJIFUNZE NA WAO”.


No comments:

Post a Comment

              2021-MWAKA WA AKILI INAYOPITA MIPAKA Kingdom Business Clubaship  leo Tumeingia Mwaka 2021, Kila Mwaka Tarehe Moja Ya Mwezi Wa ...