Monday, June 26, 2017

The Friends of God

19th June, 2017.

THE LOVE OF GOD AND PEOPLE (Mathayo 22:36-40)

KINGDOM JOBS (Mathayo 9:36-37)

TIME & BUSINESS COACH

Title: THE FRIENDS OF GOD/MARAFIKI WA MUNGU

  2 Wakorintho 5:7

  Waebrania 11:6,;10:38

  Warumi 10:7

  Zaburi 11:3


Chanzo cha mwanadamu ni Mungu kwa kuwa maandiko yanasema “Mungu akasema Na tumfanye mtu kwa mfano wetu… Mwanzo 1:26” na akasema sisi tu miungu wadogo ndiyo maana tu marafiki wa Mungu. Yesu Kristo alisema hatatuita tena watumwa bali marafiki- sisi tu kaka na dada wa Yesu Kristo(Waebrania 2:11-KJV),Wagalatia 4:7. Wewe ni rafiki wa Mungu, na ili uwe rafiki wa Mungu lazima uweze kutawala na Yeye.

Ili upate kazi lazima uwe rafiki wa Mungu kwanza kama ilivyo kwa kampuni Fulani uendapo kuomba kazi lazima umjue mtu Fulani mwenye nafasi ya juu ili upate kazi kwa kampuni hiyo. Kama baba yako hakuwa na jina kubwa nchini au eneo uishilo ni vigumu kupata kazi ndiyo maana lazima uwe rafiki wa Mungu kwanza kabla hujaenda kwenda kuomba kazi. Kama una tengeneza urafiki wa fedha na fedha na ikatokea ukaishiwa hakika utakufa! Ukiwa rafiki wa Yesu Kristo hutembei na Fedha, watu wengi wana urafiki na yule mwovu kwa maana hupenda pesa mno kuliko Mungu.
2 Wakorintho 5:7, huwezi kumpendeza Mungu kwa kuona tu kwa kuwa ukitaka kutengeneza urafiki na Mungu vitu vyako vyote lazima  vianze na kwenda kwa Imani(Kuona rohoni mwako). Watu wengi wanaoteseka duniani leo ni wale wanaoishi kwa kuona hasa kwa mambo ya mwilini. Na ikitokea kila kitu ukitaka kufanya mpaka uanze kwa kuona kwanza utakuwa unafanya vitu vyako kwa kiwango cha hali ya chini sana“slow sana”
Vitu vinavyo mtenganisha mtu na Mungu ni kama ifuatavyo;
  1. Sin/dhambi- Warumi 6:23
  2. Ignorance/Ujinga- Hosea 4:6
  3. Fear/Hofu- 2 Timotheo 1:7
  4. Shame/Aibu-  Waebrania 12:2
Ili uwe urafiki na Mungu lazima kwanza uanze kufanya vitu viwili tena iwe mwendelezo;
  • Repent/tubu-Mathayo 4:17, Matendo 3:19, Tafuta Mistari ya Toba, Tafuta Neno la kusimamia.
  • Think through the Word of God/Fikiri kwa kupitia Neno-Joshua 1:8, Facts and Truth ndilo Neno la Mungu.
Mungu akiongea anaumba, mwanadamu akiongea ana fikiri kupitia Neno lake (la Mungu). Vifuatavyo ni vyanzo ya kufikiri:
  1. Kufikiri kupitia Neno la Mungu
  2. Kufikiri kupitia umbaji wa Mungu
  3. Kufikiri kwa Kupitia kazi ya Adamu (Mwanzo 2:15) na Kazi ya Yesu (Mathayo 1:21, 6:33) Kupitia kazi hizi mbili za Adam na Yesu utaona unaanza kuhudumiwa na Malaika. Utakapoanza kumrudishia Mungu Muda wako ndipo malaika wataanza kukuhudumia.

HITIMISHO
Aibu rafiki yake mkubwa ni hofu. Hofu na aibu siyo Imani, jifunze kujifunza kufuta dhambi mara kwa mara ili ujinga, hofu na aibu viondoke.
Mithali 10:22, fedha chafu hununua vitu vichafu, fedha safi hainunui vitu vichafu na mtu hatajiriki na pesa bali Baraka zitokazo kwa Mungu. Acha kutegemea nature”asili” tegemea huduma ya Malaika…eti msimu huu ni msimu wa maembe, acha kutegemea vitu vya asili.


Unaswali/Maoni/Mapendekezo komenti hapo chini au Una ushuhuda usisite kutuandikia Kupitia hapa au kwa rewiew section ya Facebook (Tazama kwenye ukurasa huu utaziona nyota hivi, ziweke upendazo baadae andika hapo-Asante.)





No comments:

Post a Comment

              2021-MWAKA WA AKILI INAYOPITA MIPAKA Kingdom Business Clubaship  leo Tumeingia Mwaka 2021, Kila Mwaka Tarehe Moja Ya Mwezi Wa ...