Monday, September 18, 2017

The Seed of Business

17th September, 2017.
THE LOVE OF GOD AND PEOPLE (Mathayo 22:36-40)
JESUS IS LORD
KINGDOM BUSINESS CLASS (Mathayo 6:33)
TIME & BUSINESS COACH
Title: THE SEED OF BUSINESS/MBEGU YA BIASHARA
LUKA 8:11
YOHANA 1:1-5
LUKA 2:49

Mbegu nini?
Mbegu ni sehemu ya chanzo cha kitu fulani inaweza ikawa tunda la mmea ukaendelea na kuwa mmea mpya. Mbegu ni njia ya kuzaa vitu vingi ndani ya muda kama ilivyo Mbegu ya mmea inaanzishwa ndani ya ua la mmea inaendelea kukua na ndivyo ilivyo maisha ya mwanadamu utajiri au mafanikio yake yapo ndani ya muda.
Mungu alipoziumba mbingu na dunia kila kitu ndani yake aliweka mbegu siyo tu katika miti, mimea,majani na wanyama hata binadamu pia aliweka mbegu zake ili kuendeleza uzao wa jambo husika kwa kila masaa 24 yapewayo dunia hii. Hivyo basi kitu chochote unataka kufanya duniani humu lazima upande mbegu kwanza chini ikiwa ni ardhini, kwenye biashara au muda n.k
Lk 8:11, Yohana 1:1-15:14, swali la msingi la kujiuliza kwa mfano unahitaji fedha nyingi uzishike mkononi mwako wewe sasa umetoa fedha kiasi gani kwa watu wasiojiweza “NGO” kulingana na kitabu cha Yakobo 1:27? Unata kuishi miaka mingi hapa duniani ume mrudishia Mungu masaa mangapi unapoendelea kuishi?
Swali la msingi la kujiuliza unapandaje mbegu sasa? Mbegu zinapandwa kwa aina mbili kuna zile unapanda shambani hizi huoza na kuota mmea na zile ambazo unapanda kwenye akili za watu(kuwapa mafunzo kama ilivyo huduma hii ya Kingdom Business). Mbegu hizi huwa hazifi kabisa utazivuna kwa wakati usio jua ‘mbegu za kiroho’. Napenda utambue ya kwamba utajiri mkubwa duniani ni ule ambao unapandwa vichwani mwa watu ‘akilini’ kupitia taarifa “information” unazo toa kwa watu husika. Zifuatazo ni mbegu zinazo tumika hapa duniani
  1. The word of God/Neno la Mungu
  2. Time/Muda-kila masaa 24
  3.  Project Seed/Mbegu ya Mradi
  4.  Seed money/Mbegu ya pesa
  5. The seed of a Man/Mbegu ya mwanadamu
  6. Plants or fruits seed/ Mimea au mbegu za matunda
Katika mpangilio huu hapo juu namba moja ndiyo  jambo la kwanza katika mambo yote ‘NENO LA MUNGU’. Kupitia Neno huzaa maneno yanayoweza yakawa ni giza la yule mwovu au Nuru ‘NENO LA MUNGU ni sawa na kusema laana au baraka. Watu wengi wanateseka leo kwa sababu ya labda ya maneno waliyosema au waliyo nenewa na watu na wao hawakuyatengua yakawa giza baadae ikawa laana kwao. Futa mbegu za laana ulizo nenewa na watu au wewe menyewe ulizo jinenea na uanze kumshukuru Mungu katika kila jambo.
WORD FOR WORD
Neno kwa Neno ni maneno ya Baraka au laana jinsi unavyo ongea maneno mengi yakiwa ya kiovu ndivyo utakavyo jilaani mwenyewe. Nenda kinyume na maneno kama haya:
Challenge/Changamoto=Nenda na  Neno THANKSGIVING/SHUKRANI
Temporary/ya muda mfupi=Nenda na Neno Testimony/Shuhuda
Ikitokea ukaona mambo hayaendi wala haufanikiwi cha kwanza utambue ya kuwa Mungu hampi mtu vitu viwili kwa wakati mmoja, lazima kimoja ukiachie ili upate kingine. Kwa uwelewa tu wa haraka haraka Mungu hawezi kukupa fedha na Muda kwa wakati mmoja. Atakupa muda ili utafute fedha au fedha atakupa ili uukomboe muda.
Kila masaa 24 unayopewa ya siku husika ni mbegu na inatakiwa uipande labda shambani au vichwani mwa watu. Hapa duniani watu wameletwa au kuumbwa kwa aina mbili.
  1.  Kuna Watu ni MBEGU na
  2.  Kuna Watu ni MKATE
SEED AND BREAD
God doesn’t look for beggars but partners/ Mungu hatafuti ombaomba”wa mkate” bali washirika wa kushirikiana Naye “mbegu”
Kitu cha ajabu leo hii watu wengi ni “MKATE” ijapo kuwa waliletwa duniani kama Mbegu na si mkate. Ni kweli kabisa kuna huu mstari “Utupe leo riziki yetu” Mathayo 6:11 Tafsiri ingine husema “Utupe leo Mkate wetu wa kila siku” tena mstari huu husemwa kwenye Sala ya Baba Yetu. Mstari huu uliwekwa kwa ajiri ya mtu mchanga kiroho wewe kama umekuwa kiroho sema “Utupe leo mbegu yetu!”

SIFA ZA MBEGU
  1.  Seed never afraid to die/ Mbegu haiogopi kufa, Yohana 12:24
  2. Seed produce seed/ Mbegu huzalisha mbegu
  3. Seed never afraid copy and paste
  4. Seed gives ideas to people/ Mbegu hutoa wazo kwa watu
  5. Seed put others first/ Mbegu huweka wengine kwanza
  6. Seed uses its own faith/ Mbegu hutumia imani yake yenyewe
  7. Mbegu haina hofu wala woga au aibu
  SIFA ZA MKATE
  1.  Mkate hua ribika kwa haraka ‘hufa’ hauna mbegu “haizalishi nyingine”
  2. Mkate hujari sana mambo ya mwilini,Wagalatia 5:19-21
  3. Mkate HAUNA VIFUATAVYO Upendo, Furaha, Amani, Uvumilivu, Utu wema, Fadhili, Uaminifu, Upole, Kiasi.
  4. Mkate hujari na kuweka mambo yake kuwa ya kwanza tu na si ya wengine.
  5. Mkate hutoa mawazo hasi pamoja na kutumia imani ya mtu mwingine
  6. Mkate hukopi na kupaste kutoka kwa mwingine na huogopa kufa
  7. Makate una hofu,uwoga na aibu
JIPIME MWENYEWE JE WEWE NI MBEGU AU MKATE?
HITIMISHO
Uanzishapo biashara lazima uwe na neno litakalo leta wazo la kuanzia nalo katika biashara yeyote ile “THE SEED OF BUSINESS” huku ukiandika chini wazo husika. Toa muda wako ili kuzalisha fedha kwa sababu fedha na muda ni MBEGU YA BIASHARA.

 Una swali/Maoni/Mapendekezo komenti hapo chini au Una ushuhuda usisite kutuandikia Kupitia hapa au kwa rewiew section ya Facebook  (Tazama kwenye ukurasa huu utaziona nyota hivi, ziweke upendazo baadae andika hapo-Asante.)





No comments:

Post a Comment

              2021-MWAKA WA AKILI INAYOPITA MIPAKA Kingdom Business Clubaship  leo Tumeingia Mwaka 2021, Kila Mwaka Tarehe Moja Ya Mwezi Wa ...