Monday, August 28, 2017

THE ENOUGH FAITH/IMANI INAYOTOSHA



27th August, 2017.

THE LOVE OF GOD AND PEOPLE (Mathayo 22:36-40)

JESUS IS LORD

KINGDOM BUSINESS CLASS (Mathayo 6:33)

TIME & BUSINESS COACH

THE ENOUGH FAITH/IMANI INAYOTOSHA

Rum 10:17

Rum 14:2

Rum 14:23

Ebr 11:1

Imani nini?
“Kuwa na Imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona” Kutoka Biblia ya Habari njema. Katika Imani kuna ngazi kuu mbili

  •             Kuamini Imani (KUSIKIA+IMANI+STORY= KUAMINI      
  •              Kujua IMANI (IMANI+STORY+NAMBA”MUDA”= Ebr 4:2

Unaweza ukaamini lakini kisitokee Ila UKIJUA “Ukijua Imani” kitu hicho kitatokea kwa vile una tumia muda “una cheza na namba baada ya kusikia,Imani yenyewe, story yako na muda unao kipa hicho kitu mwishoe kitatokea. Imani ni mfumo wa fedha wa mbinguni, pale fedha ikishindwa kununua kitu fulani imani ndiyo inachukua nafasi. Unapo angalia vitu au fedha ikashindwa angalia Imani uliyo nayo. Kwa bahati mbaya sana leo hii watu wengi wakipungukiwa au wakiwa hawana fedha mifukoni mwao huishiwa na nguvu kila mahali na kuona maisha yamekuwa magumu sana pasipo fedha.

Ukiwa na Imani iliyo jitoshereza shida ikitokea na imani uliyo nayo ni kubwa ujue utashinda tu. Ukiwa huna imani hofu huingia na hofu ni mama yake na uwoga na baba wa uwoga ni aibu. Kuna aina tatu za kiwango cha imani
  1.    Neno la Imani/ The word of Faith- Rum 10:17 “Mkristo mchanga”
  2.   Karama ya Imani/ The gift of Faith- 1 kor 12(soma yote), “Watumishi wengi wapo hapa”
  3.   Roho ya Imani/ The spirit of Faith “Roho aliyokuwa nayo Kristo-Watumishi wakubwa wanayo hii roho, wakisema vitu vinatokea.

Kiwango cha imani kikijitosheleza utakula au kunywa kila kitu “ Watu hutofautiana: Mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.” Warumi 14:2(BHN). Kiwango chako cha imani kinaamua jinsi ya kufanya maamuzi yako “the power of decision/nguvu ya kufanya maamuzi”
Mungu hafanyi kazi na walio na ulegevu kiimani. Mtu asiyekuwa na nguvu ya maamuzi kiwango chako cha imani hakitoshi. Kwa mfano walio ajiriwa hawafikirii! Wameibiwa nafasi zao na mabosi wao!

THE POWER OF DECISION MAKING
#Take Risk, jihatarishe kupitia muda wako, mali zako, na maisha yako na kama huna nguvu ya maamuzi huwezi kutoka hapo ulipo, sehemu mojawapo ya kuanza kufanyia maamuzi tambua ya kuwa umekuja duniani peke yako na duniani humu kuna wajinga wengi hautaeleweka unapotoa au kushare maono yako kwa kuwa maono hayo umepewa wewe na si wao. Imani ya watu wengi haitoshi kwa sababu wanaangalia fedha/pesa na mtu wa namna hii ameshindwa kabla hajaanza kitu.

Mthayo 11:5, Vita vya umaskini au kufanya maombi ya umaskini huwezi ukavishinda hata siku moja, hebu angalia vizazi vyako karibia vyote vimeshindwa kupambana na umaskini mwisho wake umaskini ume wauwa! nchi yetu inapambana na umaskini wewe una pambana na nini? Katika kosa kubwa linalo fanyika leo hata makanisa yana pambana na vita ya umaskini wakati mwanzilishi wa kanisa alikuja kama Mwalimu “Rabi” kuwafundisha watu ili waondokane na ujinga wa mababa zao “Tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia...-tubadilishwe nia na akili zetu”

Baba wa Taifa Mwl Julius K Nyererena  kwa ujumla duniani kipindi hicho walikuwa wanapigana na vita vikuu vitatu vya mwanzoni hapa kuanzaia namba nne ni nyongeza ya vita tuzo pigana nazo duniani leo hii-;
  1.  Ujinga/Ignorance
  2. Umaskini/Poverty
  3.  Magonjwa/maradhi/Sickness/disease
  4.  Madawa ya Kulenya/Drugs
  5.  Ushoga/Homosexual
  6.  Ugaidi/Terrorism
  7. Mtandao-“ya kijamii”/Internet
Hosea 4:6, Warumi 12:2, Isaya 11:2- katika zile Roho saba za Mungu Roho nne zinausiana na akili ambazo ni Roho ya Maarifa,Hekima, Ushauri na Ufaham. #Faith is the state of mind/Imani ina husiana na akili and  #Success comes when faith is greater than time or with good deeds the faith is greater than time. Kwa mfano unataka kupika ugali ukaanza kupika tu na ukatambua ya kuwa unga ni mdogo utakunywa uji hakika!

#Don’t compete with people compete with time/shindana na muda na si watu/. #Overcome your time with good characters/ uushinde muda kwa tabia njema. #The greatest partner is your time/Muda ndiyo rafiki yako wa karibu huwezi kuachana naye! #Time is a person with your personality, muda unaongea- #One habit of time is dying every second, it has a human character/Moja ya tabia ya muda una kufa kila sekunde, una tabia ya mwanadamu.

Kusoma Neno la Mungu linaongeza kiwango chako cha imani ndipo ujinga utaondoka lakini ukipigana vita vya umaskini hakika utakufa mapema kabla ya muda wako! Kwa kuwa Mungu hampi pesa/fedha mtu mijnga hata siku moja mpaka upate maarifa kwanza ili uondoe ujinga “Hosea 4:6”, unataka kuwa tajiri wa mali nyingi tatua matatizo makubwa ya watu wengi, ongeza maarifa mengi kila sekunde upumuayo. Ukipigana na umaskini utakuwa una tafuta fedha na ukipambana na ujinga utakuwa unatafuta pesa “kuna tofauti kati ya pesa na fedha, fedha ni hizi za sarafu na noti tunazoziona na Pesa ni roho kwa lugha nyingine inaonekana kwa makaratasi kama ilivyo mfumo wa benki huendeshwa kwa kutumia makaratasi!

Kitabu cha Mhubiri 10:15(BHN), Uki kaa na watu wanaopigana na umaskini utajikuta na wewe unapigana vita hivyo hivyo kama ilivyo vita vya ujinga nawe utajikuta unapigana na vita vya Ujinga. Mwisho kabisa ukitaka usiwe mzee mapema pigana vita vya ujinga lakini ikatokea unapigana na vita vya umaskini uzee una kukaribia haraka!

HITIMISHO
Imani iliyo jitosheleza, ikatokea kama unafanya biashara “hauja uza” unasemaje? Ukisema umelogwa au ni hila za mwovu ujue unapigana na vita vya umaskini ondoka hapo haraka. Asilimia 80 katika maisha ya mwanadamu anafanya kwa sababu ya tamaa za mwili na kwa asilimia 20 zilizo baki kwa kupia mapepo! Takwimu hizi ni kwa yule asiye tumia akili ya Mungu kwa maana Mungu anaposema “tusi zitegemee akili zetu wenyewe” ana maanisha “tutumie akili ya Mungu pekee” –usitumie akili yako=TUMIA AKILI YAKE, kwa mfano mtu ana kwambia usilipe maana yake yeye ata kulipia.

 Unaswali/Maoni/Mapendekezo komenti hapo chini au Una ushuhuda usisite kutuandikia Kupitia hapa au kwa rewiew section ya Facebook  (Tazama kwenye ukurasa huu utaziona nyota hivi, ziweke upendazo baadae andika hapo-Asante.)

























No comments:

Post a Comment

              2021-MWAKA WA AKILI INAYOPITA MIPAKA Kingdom Business Clubaship  leo Tumeingia Mwaka 2021, Kila Mwaka Tarehe Moja Ya Mwezi Wa ...